Rais wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Leodegar Tenga amekataa barua ya
kuomba kujiuzulu ya Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi ya TFF, Said Mohamed.
Mohamed
ambaye ni Mwenyekiti wa klabu ya Azam alimuandikia Rais Tenga barua ya
kujiuzulu wadhifa huo akipinga kauli ya Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya TFF,
Alfred Tibaigana juu ya adhabu zilizotolewa na Kamati ya Ligi kwa baadhi ya
wachezaji wa Yanga.
Rais Tenga
amesema alimteua Mohamed katika Kamati hiyo kwa kuzingatia uadilifu wake na
uwezo wake katika kuongoza, hivyo amekataa barua hiyo ya kuomba kujiuzulu.
Kwa mujibu
wa mamlaka aliyopewa na Mkutano Mkuu wa TFF, Rais Tenga, Oktoba 28 mwaka jana
aliunda Kamati ya Ligi ambayo wajumbe wake wanatoka kwenye klabu za Ligi Kuu ya
Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza.
Wajumbe wa
kamati hiyo ni Wallace Karia (Mwenyekiti), Said Mohamed (Makamu Mwenyekiti),
Damas Ndumbaro, Steven Mnguto, Geoffrey Nyange, Seif Ahmed, Henry Kabera, ACP
Ahmed Msangi, Meja Charles Mbuge na Ahmed Yahya.
No comments:
Post a Comment